Psalms 14

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 53)

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Zaburi Ya Daudi)


1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.


2 b Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.

3 cWote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!


4 dJe, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Bwana?

5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

6 eNinyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
bali Bwana ndiye kimbilio lao.


7 fLaiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Bwana arejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!
Copyright information for SwhKC